HAWA NDIO WALIOIUA JUVENTUS BERLIN
MIAMBA ya kandanda ya Hispania,
FC Barcelona imefanikiwa kutwaa kombe la tano la Uefa Champions League
baada ya kushinda 3-1 dhidi ya mabingwa wa Italia, Juventus katika mechi
ya fainali iliyopigwa usiku huu uwanja wa Olympic, mjini Berlin,
Ujerumani.
Barcelona walianza mchezo kwa
kasi huku wakigongeana pasi za uhakika na katika dakika ya tatu, Ivan
Rakitic aliandika bao la kwanza akimalizia pasi murua ya Andres Iniesta.
Bao hilo lilidumu hadi kipindi cha kwanza kinamalizika.
Kipindi cha pili Juventus
walijipanga na kusawazisha goli hilo kupitia kwa Alvaro Morata
aliyemalizia mpira uliotemwa na golikipa kutokana na shuti kali la
Carlos Tevez.
Dakika ya 68′ Lionel Messi
alipiga shuti kali lililotemwa na kipa wa Juve, Buffon na mpira kumkuta
Luis Suarez aliyefunga goli ta pili na la ushindi.
Dakika za nyongeza, Neymar akaifungia Barcelona goli la tatu kutokana na shambulizi la kushitukiza.
Barcelona chini ya Luis Enrique
wamefanikiwa kutwaa makombe matatu msimu huu kwani awali walitwaa La
Liga na kombe la Mfalme ‘Copa del Rey’.
Hakika msimu wa 2014/2015 ulikuwa mgumu kwa walinzi wa timu za La Liga na Uefa Champions League kwasababu moto wa Lionel Messi, Luis Suarez na Neymar Jr ni sawa na wa Petroli usiozimwa kwa maji.
Hakika msimu wa 2014/2015 ulikuwa mgumu kwa walinzi wa timu za La Liga na Uefa Champions League kwasababu moto wa Lionel Messi, Luis Suarez na Neymar Jr ni sawa na wa Petroli usiozimwa kwa maji.
No comments:
Post a Comment